March 16, 2022

MWENYEKITI WA HALMASHAURI (W) LUDEWA,ANENA NENO




Mwenyekiti wa Halmashauri Wilaya ya Ludewa Wise Mgina Jana Machi 15, 2022 alitembelea Msitu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ulioko Kata ya Madope ambao uliungua na moto mwishoni mwa mwaka 2021.

Katika hatua nyingine Mhe. Mwenyekiti Wise Mgina alipo kuwa akikagua msitu huo alisema kuwa,"Msitu huu ni msitu ambao ulikuwa ni sehemu ya utajiri wa Halmashauri yetu,lakini moto ulivamia na kutuingiza hasara ya kuanza kuvuna miti hii kwa muda usio pangwa.


Mhe.Mgina aliongeza kwa kusema kuwa,Licha ya hasara ambayo imejitokeza hatuwezi acha miti hii ikauke,sisi kama Halmashauri tumeamua tuuchane mbao wenyewe.

Ikumbukwe kwamba Mwezi Januari 10 Mwaka huu Halmashauri ilitangaza kuuzwa kwa miti hiyo ambapo walijitokeza wanunuzi mbalimbali na kutaka kuununua kwa bei chini na uongozi wahalmashauri haikusita kusitisha kuuza msitu huo kwa hasara.


Hali kadhalika Mheshimiwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Wise Mgina aliongeza kwa kusema kuwa,Wengi wamekuja wakitaka kununua miti hii iliyo ungua kwa bei ndogo lakini sisi kama Halmashauri tumekataa tumeamua kuuchana wenyewe,kwa hatua hii tulio ichukua tunatarajia kupa mbao zaidi ya 50,000 zinapatika hapa,na mbao hizi zikipatikana zitatumika kwenye majengo ya Serikali yanayo jengwa sasa na yatakayo jengwa baadae.

Pia alimaliza kwa kusema kuwa' wananchi wote wa Wilaya ya Ludewa natumia nafasi hii kuwasihi acheni kuchoma moto ovyo, mnairudisha halmashauri yetu nyuma kwa kuharibu miti,ipo miti mingi ndani ya Halmashauri hii imeungua na haijafikia kiwango cha kupasuliwa tufuate taratibu za kupata kibali cha kuchoma moto kutoka kwenye serikali ya vijiji vyetu.


2 comments:

  1. Ni muhimu sana kutunza rasilimali zetu dhidi ya majanga ya kuepukika kwa faida ya watu wetu kwa sasa na kizazi kijacho.

    ReplyDelete

FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA

Wakati ukijiuliza wapi zinapatika fursa za kilimo hapa nchini Tanzania leo nakunong'oneza kwa ukaribu kuwa Halmashari ya Wilaya ya Ludew...