Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndg. Sunday Deogratias anawajuza wananchi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kuwa, katika zoezi la Utoaji elimu ya mfumo wa anwani za makazi kwa Watumishi wote wa Tarafa 5 watakao waongoza vijana walio chaguliwa kutoka kwenye kata zote za Wilaya ya Ludewa limekamilika Jana Machi15, 2022.
Aidha anapenda kuwajuza kuwa, zoezi linalo fuata sasa ni kuwapa semina elekezi ya namna ya kuchukua taarifa kwa usahihi na kuzitunza katika mfumo.
Vijana wote wenye sifa walio chaguliwa kutoka kwa watendaji wa Kata, hivi karibuni mtapewa taarifa ya lini na muda gani mtapaswa kuja kupewa semina.
Lakini pia Ndg Sunday Deogratias anawaomba wanachi wote pindi vijana hao watakapo anza kupita kwenye makazi yao kwaajili ya kuchukua taarifa muwape ushirikiano ili kukamilisha zoezi hili kwa muda ulio pangwa.
Usisahau kutembelea kurasa zetu za mitandao ya kijamii {Twitter "Halmashauri Ludewa" Blog "Halmashauriludewa.blogspot.com" na YOU TUBE CHANEL kwa jina la "Halmashauri Ludewa".
No comments:
Post a Comment