March 19, 2022

LUDEWA NI WILAYA ILIYO BARIKIWA NCHINI TANZANIA



Ninapo zungumzia Fursa za Uwekezaji ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ninamaanisha zipo fursa nyingi kama ifuatavyo:-

Tuko na Fursa za Kilimo
Fura ya Mifugo
Fursa za Utalii
Fursa za Madini

Wilaya yetu ya Ludewa imejaliwa kuzungukwa na ukijani mbichi kila mahali na Milima mizuri inayo vutia kuitizama na kuona kama uko Dunia ya zaidi ya Dunia.

Hapa nakuangazia tu Moja ya Vivutio vinavyo tamanisha wengi kuja kutalii na mimi pia nakukaribisha sana kuja kufanya Utalii wewe mwenyewe.

Tuko na Utalii wa Ziwanyasa,Mungu hakuacha kutupatia Ziwanyasa ukanda wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ambako sasa ni Tarafa ya mwambo,huko kuna utalii ndani ya Ziwanyasa,utakutana na maji ya aina yake ndani ya ziwanyasa,Mchanga unao patikana ziwanyasa ukanda wa Ludewa ni tofauti kabisa,Utagundua Mikondo ya maji ya ziwanyasa ni tofauti na mikondo mingine iliyo zoeleka,na kwa upande wa mawe mapambo ya ziwanyasa ndio usiseme kabisa,ukiwa kama unaelekea Mbeya kule kunako itwa Makonde hauto juta kufika kutizama milima iliyo jipanga kwa ngazi moja na nyingine.

hapo nimekusogezea vichache tu ukiondoa samaki wenye rangi alimaarufu kwa samaki wa mapambo,je Utafikaje kote huko ? jibu ni kwamba Karibu Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri utapata maelekezo yaliyo jitosheleza nami nitaambatana nawe hadi kote ukutakako

Ludewa ni Wilaya iliyo barikiwa nchini Tanzania

No comments:

Post a Comment

FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA

Wakati ukijiuliza wapi zinapatika fursa za kilimo hapa nchini Tanzania leo nakunong'oneza kwa ukaribu kuwa Halmashari ya Wilaya ya Ludew...