March 09, 2022

MKURUGENZI MTENDAJI HALMASHURI YA WILAYA YA LUDEWA ATEMA CHECHE




Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndg.Sunday Deogratias akiwa katika sherehe ya Wanawake Duniani,ambapo kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ilifanyika siku ya jana Machi 08, 2022 katika Viwanja vya sokoni Ludewa mjini aliongea na wakina mama walio jitokeza na kuwahidi kuwa serikali ipo jirani na wakina mama.

Aidha aliongeza kwa kusema kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kwa mwaka  2020/2021 imekopesha vikundi mbalimbali vya wakina mama,vijana na watu wenye ulemavu,na kwa mwaka 2022/2023 bado inaendelea kukopesha fedha kwa vikundi vyote na akawataka wakina mama wote wa halmashauri ya wilaya ya Ludewa wafike katika ofisi za Maendeleo ya jamii kusajiliwa vikundi na hatimaye wakopeshwe fedha.

,Natumia nafasi hii kuwakumbusha wakina mama wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kuwa, Halmashauri yetu inapesa isiyo na riba,jitokezeni mje mkope na sisi kama Halmashuri tupo tayaali kuwapatieni,lakini pia nanyi vijana wetu mliopo hapa pamoja na watu wenye ulemavu jitokezeni sajilini Vikundi njoeni kopeni pesa,fedha hii ipo inawasubiri ninyi wenyewe’.



Hali kadhali Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Ndg.Sunday Deogratius kupitia sherehe ya Wanawake Duniani,akawakumbusha wananchi wote wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kutumia fursa ya utajiri mkubwa uliopa Wilayani Ludewa.

Wakina mama ludewa inafunguka,Fursa ya uwekezaji ni mkubwa,Wawekezaji zaidi ya watatu tayali wamefika Ludewa na kuanza kuandaa mazingira ya kazi kwenye migodi hapa Kwenye Wilaya yetu,anzeni kuweka mipango ya kuwahudumia wageni kwa kuwauzia chakula,Jengeni nyumba za kulala wageni na kama huna pesa kwani mgahawa unahitaji mtaji wa shilingi ngapi?fuata taratibu tukukopeshe fedha ambayo haina riba,Wilaya hii inapokea wageni wengi watakosa kwa kulala watakosa kwa kula kama msipo tumia fursa hii.



Lakini pia Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa akaongeza kuwakaribisha watanzania wote walioko nje ya Ludewa na wageni wa mataifa yote kuja kuwekeza Halmashauri ya Wilaya ya ludewa.

Uploading: 5155153 of 5155153 bytes uploaded.


Ndugu zangu watanzania wote nawakaribisha Ludewa,Wilaya ya Ludewa ni salama kwa uwekezaji ziko fursa nyingi za uwekezaji,karibuni kuwekeza Ludewa,Kule Manda tuna ziwa nyasa ambalo ziwa hilo ni utalii tosha kwa Mkoa wetu wa Njombe na Tanzania kwa ujumla wake,ukienda kule Lupingu,Makonde utagundua mwambao inautalii wa kipekee hapa nchini Tanzania na duniani kote,njoo wekezeni kwa ujenzi,biashara na mambo mengine maadamu tu hauvunji sheria za nchi yetu,wazawa wa Wilaya ya Ludewa Mlioko nje ya Wilaya hii Leteni wageni wawekeze nyumbani na ninyi wenyewe Ludini nyumbani kuwekeza na kuibadilisha Ludewa,Ludewa sasa ni tajiri tunakila sababu ya kuja kufanya uwekezaji.

No comments:

Post a Comment

FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA

Wakati ukijiuliza wapi zinapatika fursa za kilimo hapa nchini Tanzania leo nakunong'oneza kwa ukaribu kuwa Halmashari ya Wilaya ya Ludew...