March 10, 2022

NEEMA YA MAJI YAMWAGIKA MADINDO

Diwani wa Kata ya Ludende Mhe.Vasco Mgimba ameishukuru Serikali ya awamu ya sita ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kufanikisha kuwapelekea maji wananchi wa Kijiji cha Madindo Kata ya Ludende Wilaya ya Ludewa.

 Akizungumza hayo Jana Machi 09, 2022 wakati akikagua miundombinu ya maji inayo jengwa na RUWASA,”Tunakila sababu ya kumshuuru Mheshimiwa Rais Kwa kuona wananchi wanavyo teseka na upatikanaji wa maji,leo maji yanatoka hivi ujue Rais kasikia kilio chetu’. Amesema  Vasco Mgimba  



 Sambamba na hayo akaongeza kwa kusema kuwa wananchi wa Kata ya Ludende sasa maji safi na salama yamepatikana wanapaswa kuilinda na kuitunza miundombinu hiyo ili isaidie kizazi cha leo na cha baadaye.



 Wananchi wa kijiji cha Mandindo Kata ya Ludende Baada ya kusubiri kwa muda mrefu kupata maji sasa mnakila sababu ya kuilinda miundombinu hii ili isaharibiwe na yeyote,Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imekelezwa hapa leo kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ya chama change, moja ya vipaumbele vyake ni kuhakikisha wananchi wanaondokana kwenye changamoto ya upatikanaji wa maji. Amesema  Vasco Mgimba

No comments:

Post a Comment

FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA

Wakati ukijiuliza wapi zinapatika fursa za kilimo hapa nchini Tanzania leo nakunong'oneza kwa ukaribu kuwa Halmashari ya Wilaya ya Ludew...