Diwani wa Kata ya Ludende Mhe.Vasco Mgimba ameishukuru Serikali
ya awamu ya sita ya Mhe.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
kwa kufanikisha kuwapelekea maji wananchi wa Kijiji cha Madindo Kata ya Ludende
Wilaya ya Ludewa.
Akizungumza hayo Jana Machi 09, 2022 wakati akikagua miundombinu
ya maji inayo jengwa na RUWASA,”Tunakila sababu ya kumshuuru Mheshimiwa Rais
Kwa kuona wananchi wanavyo teseka na upatikanaji wa maji,leo maji yanatoka hivi
ujue Rais kasikia kilio chetu’. Amesema Vasco
Mgimba
Sambamba na hayo akaongeza kwa kusema kuwa wananchi wa Kata ya Ludende
sasa maji safi na salama yamepatikana wanapaswa kuilinda na kuitunza
miundombinu hiyo ili isaidie kizazi cha leo na cha baadaye.
Wananchi wa kijiji cha Mandindo Kata ya Ludende Baada ya
kusubiri kwa muda mrefu kupata maji sasa mnakila sababu ya kuilinda miundombinu
hii ili isaharibiwe na yeyote,Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) imekelezwa
hapa leo kwa mujibu wa ilani ya uchaguzi ya chama change, moja ya vipaumbele
vyake ni kuhakikisha wananchi wanaondokana kwenye changamoto ya upatikanaji wa
maji. Amesema Vasco Mgimba
No comments:
Post a Comment