Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya leo Machi 05, 2022 amefanya ziara katika Wilaya ya Ludewa akikagua Mradi wa Ujenzi wa Majengo ya Chuo cha VETA kinacho jengwa katika Kata ya Lugarawa Kijiji cha Shaurimoyo.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya amemshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kilio cha wananchi kwa kusuasua kwa ujenzi wa chuo hicho ambapo Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ametoa fedha ya ujenzi wa chuo hicho mwanzoni mwa mwezi Januari mwaka huu kiasi cha zaidi ya Shilingi, Bilioni Tano na Milioni Mianne thelathini na tano kwaajili ya ujenzi wa majengo ya chuo hicho.
Sambamba
na hilo Mhe.Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya amemuelekeza Mjenzi
anaye jenga majengo ya chuo hicho kukamilisha majengo hayo ndani ya muda ulio
pangwa, kwa upande wake mkandarasi wa ujenzi wa chuo hicho amemuahidi Mkuu wa
Mkoa wa Njombe kuwa Ujenzi huo utakamilika kwa miezi tisa kutoka sasa.
Katika
hatua nyingine Mhe.Mkuu wa Mkoa wa Njombe amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Ludewa
na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kushiriki kikamilifu usimamizi wa mradi
huo na kuvitaka vyombo vya Ulinzi na Usalama vya maeneo hayo kulinda na kutunza
vifaa vyote vya ujenzi vikiwemo,Saruji na Nondo.
Sambamba na hilo Mhe.Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhandisi Marwa Rubirya amemuelekeza Mjenzi anaye jenga majengo ya chuo hicho kukamilisha majengo hayo ndani ya muda ulio pangwa, kwa upande wake mkandarasi wa ujenzi wa chuo hicho amemuahidi Mkuu wa Mkoa wa Njombe kuwa Ujenzi huo utakamilika kwa miezi tisa kutoka sasa.
Katika hatua nyingine Mhe.Mkuu wa Mkoa wa Njombe amemwagiza Mkuu wa Wilaya ya Ludewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kushiriki kikamilifu usimamizi wa mradi huo na kuvitaka vyombo vya Ulinzi na Usalama vya maeneo hayo kulinda na kutunza vifaa vyote vya ujenzi vikiwemo,Saruji na Nondo.
Okay,
ReplyDelete