March 23, 2022
FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA
March 22, 2022
TAARIFA KWA UUMA
Kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa
POLIO nchini Malawi, Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya
ya Ludewa itaanza zoezi la kampeni ya utoaji wa chanjo ya matone ya kuzuia
ugonjwa wa kupooza kwa watoto walio chini ya umri wa miaka mitano (5).
March 21, 2022
KAIMU MKURUGENZI WILAYA YA LUDEWA AAGIZA ELIMU YA KULIFIKIA DAWATI LA JINSIA IWAFIKIE WANANCHI ITAPUNGUZA UKATILI DHIDI YA WATOTO NA WANAWAKE
March 19, 2022
LUDEWA NI WILAYA ILIYO BARIKIWA NCHINI TANZANIA
HALMASHAURI LUDEWA YATOA VYANDUA 80 KATIKA SHULE YA WATOTO WENYE MAHITAJI MAALUM MUNDINDI
MWENYEKITI WA CCM LUDEWA ATOA TAMKO
Bw. LINUS MALAMBA ASIMAMIA SEMINA YA UGONJWA WA POLIO
Leo Machi 19, 2022 Mganga Mkuu wa Wilaya ya Ludewa atoa semina ya Mafunzo kwa Kamati ya Msingi ya Afya ngazi ya Jamii (PHC) na Mgeni Rasmi akiwa ni Mkuu wa Wilaya ya Ludewa akiliwakilishwa na Kaimu Das Wilaya ya Ludewa Bw. Linus Malamba
MKURUGENZI WA SHIRIKA LA PADECO AISHUKURU HALMASHAURI YA WILAYA YA LUDEWA
March 18, 2022
MHE.WISE MGINA ATOA NENO LA NEEMA SHULE YA WATU WENYE MAHITAJI MAALUM
Mkurugenzi
Mtendaji wa Halmashauri ya Ludewa Ndg.Sunday Deogratius akiwakilishwa na Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Gilbert Ngailo amekabidhiwa bweni moja la wanafunzi wa
wakiume katika Shule ya Msingi Mudindi ya watoto wenye mahitaji maalum iliyo
jengwa na Shirika la PADECO lenye thamani ya shilingi 53,236,000/=.
Aidha shirika
la PADECO licha ya kumkabidhi Kaimu Mkurugenzi bweni hilo likiwa limekamilika
wamemkabidhi bweni likiwa na vitanda pamoja na magodoro 50 na pikipiki mpya moja
yenye thamani ya shilingi 3,800,000/=
Kwa upande wake
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Ludewa Ndg. Gilbert Ngailo amesema kuwa,
kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa amepokea
bweni hilo likiwa na vitanda na magodoro pamoja na pikipiki itakayo tumika
katika shule hiyo.
Sambamba na hayo Kaimu Mkurugenzi amempongeza Mkurugenzi wa Shirika la PADECO Ndg. Wilbard Mwinuka kwa uzalendo mkubwa anao ufanya kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa haswa katika miradi ya kimaendeleo.
Sambamba na hayo Mhe.Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa Wise Mgina ambaye pia ndiye Diwani Kata ya Mundindi amelipongeza Shirika la Padeco kwa mchango wao mkubwa haswa katika kufanikisha ujenzi wa bweni hili utakao saidia watoto wanao soma katika shule hiyo ya msingi ya watu wenye ulemavu.
Lakini pia akaongeza kwa kusema kuwa Shule hii ya watoto wenye ulemavu kwa Wilaya yetu ya Ludewa inapokea watoto kutoka maeneo tofauti nikiwa na maana ya ndani ya halmashauri ya Wilaya yetu na Mkoa mzima wa Njombe na pia saivi shule hii inapokea watoto kutoka nje ya Mkoa wa Njmbe,hivyo PADECO mchango wenu huu ni mkubwa tunawaomba msichoke kuja kuleta msaada na mahitaji mengine kadri mnavyo jaliwa.
Aidha ameongeza kwa kusema kuwa licha ya Shirika la Padeco kujenga bwini hili na serikali yetu pia imejenga jengo lingine kubwa ambalo lipo hatua za mwisho,hivyo nikiwa kama Mwenyekiti wa Halmashauri kwa umuhimu wa Shule hii,serikali inakila sababu ya kuona umuhimu wa kuongeza walimu katika shule hii ili waweze kutosheleza kuwahudumia watoto hawa,sambamba na hayo nitaenda kuishawishi serikali ione umuhimu wa kujenga na sekondari hapa,maana eneo bado lipo kubwa,na linauwezo wa kutosheleza kujenga shule ya sekondari ya watu wenye mahitaji maalumu,hii itasaidia mwenendo mzuri kwa wanafunzi wanao faulu kujinga na kidato cha kwanza,na sio hivyo tu bali nitaishawishi serikali kujenga chuo cha ufundi cha watu wenye mahitaji maalum ili waweze kujifunza mambo mbalimbali.
Kwa upandewake mwenyekitiki wa chama cha mapinduzi CCM Ndg.Stanley Kolimba amesema kuwa,PADECO wanafanya mambo mengi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa haswa katika Miradi ya Maendeleo ya Afya,Elimu,Maji na mambo mbalimbali,sisi kama chama cha mapinduzi tunawapongeza Shirika la Padeco kwa kuona Umuhimu wa kuisaidia Wilaya ya Ludewa kwa Miradi mbalimbali na mambo haya mnayo yafanya PADECO ni mambo makubwa na yakuishi,hivyo nitumie nafasi hii kuwapongezeni.
Pia Mkurugenzi wa shirika la PADECO Ndg.Wilbard Mwinuka amesema kuwa,Sisi kama shirika lisilo la kiserikali,tumefanyanya mambo mengi kwenye Halmashauri ya Ludewa ikiwepo miradi ya ujenzi wa Vituo vya Afya,Ujenzi wa Vyumba vya Mdarasa na kusaidi a vikundi mbalimbali kwa kuviwezesha vifaa na mitaji ya kuanzia kazi.
Lakini kama shirika hatuchoki kuendelea kutenda matendo ya huruma sehemu mbalimbali ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa na nje ya Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa.
March 17, 2022
LUDEWA TWAMKUMBUKA Dkt.JOHN POMBE MAGUFULI
JE , WAJUA KUWA KUTO FUATA RATIBA YA KULA HUATHIRI AFYA YA MWILI?
Ulaji mbaya wa chakula ni moja ya athari ambayo huathiri afya zetu na hapa ndipo watu wengi wana angukia, kuna makundi mawili ya ulaji mbaya wa chakula:-
1. Ratiba mbaya ya kula chalula.
Watu wengi hawana ratiba nzuri ya kula na wengi huchelewa kula kwa madai kazi zina watinga. Lakini ukweli ni kuwa ukichelewa kula una ua mwili wako taratibu, magonjwa kama vidonda vya tumbo yamekua yaki wasumbua watu wengi kutokana na kushindwa kula kwa wakati.
Kula usiku sana hupelekea mwili kutunza mafuta na ku ongezeka uzito. Kupoteza uwezo wa kufikiri,na kusinyaa kwa ubongo kutokana na kukosa cha nguvu kwa muda mrefu.
2. Kula vyakula hatarishi
Ulaji wa vyakula vya sukari kwa wingi,chumvi na kahawa hupelekea magonjwa kama shinikizo la damu na kusukari pia kuongezeka uzito kupunguza uwezo wa moyo kufanya kazi na kuathiri uwezo wa kufikiri.
Hivyo kwa nafasi hii ya kipekee nikukumbushe Mwananchi wa Wilaya ya Ludewa na Watanzania wote kwa Ujumla wake,ili kuepuka mathara yatokonayo na ulaji mbaya wa chakula, unachotakiwa kufuata ratiba ya kula, pia kuacha mara moja kula vyakula hatarishi.
MAANDALIZI YA KUUPOKEA MWENGE WA UHURU WILAYA YA LUDEWA YANAENDELEA
March 16, 2022
WANANCHI LUDEWA TWAUNGANA NA Mhe. RAIS SAMIA SULUHU HASSAN
MWENYEKITI WA HALMASHAURI (W) LUDEWA,ANENA NENO
LUDEWA YAPIGA HATUA ANWANI ZA MAKAZI
March 10, 2022
NEEMA YA MAJI YAMWAGIKA MADINDO



March 09, 2022
LUDEWA YAJIPANGA KUPOKEA MWENGE WA UHURU KWA KISHINDO 2022
Mwenge wa Uhuru unaashiria nuru na mwanga.Uliwashwa kwa mara ya nchini
Tanzania juu ya kilele cha mlima Kilimanjaro mwaka 1961.
Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2022 unatarajiwa kuwashwa rasmi Aprili 02,
2022 na Mwenge huo utawashwa katika Mkoa wa Njombe na baada ya hapo kuanza
rasmi kukimbizwa kwenye Wilaya za Mkoa wa Njombe na hatimaye kuukabidhi rasmi
katika Mkoa wa Ruvuma pale daraja la Ruhuhu lililopo Wilaya ya Ludewa.
Na kwa mwaka huu 2022 mwenge huu utakimbizwa mikoa yote nchini Tanzania na
kwa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa unatarajiwa kukimbizwa Aprili 07, 2022.
Mwenge huu unamulika nchini na nje ya mipaka ili kuleta matumaini pale
ambapo kuna kukata tamaa, upendo pale kwenye chuki na heshima pale penye
dharau.
Sisi wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa tupo tayali kuupokea
mwenge wa uhuru kwenye Wilaya yetu na Kuilinda Amani na kudumisha Upendo.
Kila mwaka kuna mbio za mwenge zinazoanzia kwenye mikoa tofauti
kuwakumbusha Watanzania jukumu lao la kulinda uhuru, umoja na amani ambavyo
vimekuwepo na kudumu.
Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kwa kutambua umuhimu na wajibu wetu wa
kulinda Uhuru Umoja na Amani ndani ya Halmashauri yetu tunasema karibu Mwenge
wa Uhuru Wilayani Ludewa,tupo tayali kuiangazia miradi ya kimaendeleo mikubwa
iliyo kamilika,inayo endelea na inayo tarajiwa kuanza.
Mwenge wa Uhuru kwa mawaka 2022 unakimbizwa ukiongozwa na kauli mbiu
isemayo,SENSA YA WATU NA MAKAZI:SENSA NI
MSINGI WA MIPANGO YA MAENDELEO,SHIRIKI KUHESABIWA,TUYAFIKIE MAENDELEO YA TAIFA.
Sambamba na hayo mengi mazuri ya ujio wa mwengi kwenye Wilaya yetu ya
Ludewa,Tunaendelea na utoaji elimu kwa kila idara ambapo siku hiyo ya Mwenge
unapo wasili kwenye Wilaya yetu ya Ludewa tutatoa taarifa ya namna ambavyo
tunaendelea na utoaji elimu na Mapambano dhidi ya VVU/UKIMWI,MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA,MAPAMBANO DHIDI YA MADAWA YA
KULEVYA,MAPAMBANO DHIDI YA RUSHWA,JINSI WILAYA INAVYO ELIMISHA WANANCHI KUHUSU
LISHE,MATUMIZI SAHIHI YA TEHAMA.
Kwa kauli hii ni dhaili Wilaya ya Ludewa tumejipanga vyema kuupokea
Mwenge wa uhuru na kuukaribisha uangaze kila pembe ya Wilaya ya Ludewa.
Mwenge wa uhuru kwa mwaka 2022 ndani ya Halmashauri yetu utakesha
ukiangaza katika kata ya Manda kule kwenye kivutio kikubwa nchini Tanzania cha
Ziwa nyasa ukanda wa Ludewa.
Ni jukumu letu watanzania wote kuupokea mwenge wa uhuru na kuendelea
kudumisha Amani na Upendo tulio izoea kwenye nchi yetu nzuri ya Tanzania na
kutokomeza Ukatili,Ukabila,udini na rangi.
Ludewa ni Wilaya inayo funguka kwa uwekezaji na kwa nafasi hii nakuomba
wewe mtanzania mwenzangu karibu Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa,tunaviongozi
mahiri na shupavu na weredi katika majukumu yao,wakiongozwa na Mheshimiwa Mkuu
wa Wilaya ya Ludewa Andrea Tsere na msimamizi na mtendaji mkuu wa Halmashauri
hiyo si mwingine bali ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa
Ndg.Sunday N. Deogratias
Mimi Chrispin Bernad Kalinga najivunia kuwapo Halmashauri ya
Wilaya ya Ludewa na ndio maana nimeona sasa nikupitishe kidogo ili uone shauku
ya kuja Ludewa,Miundombinu bora ya barabara,huduma za kijamii bila kusahau masuala
ya Afya kwenye Halmashauri yetu na nisipo gusia kwa uchache vivutio vya utalii
nitakuwa sijatenda haki.
Halmashauri yetu ya Wilaya ya Ludewa inafursa nyingi za uwekezaji
ikiwemo Kilimo,Ufugaji,Uvuvi na kubwa zaidi tunajivunia kuwa na Migodi mikubwa
ya Madini,Makaa ya Mawe,Chuma nk.
Halmashauri yetu inavivutio vingi vya utalii ambavyo sio rahisi
kuvimaliza vyote kwa ukrasa huu nitakuangazia vichache tu na,Kila kata ya
Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa inautalii wake na kuvifanya vivutio vya Utalii
kuwa vingi na kuto tamani kuondoka Ludewa,tunajivunia kuwa na Mlima mkubwa wa
Livingstone,ambapo ndani yam lima huo kunavivutio vingi vya utalii yakiwemo
mapango,wanyama,ndege wadudu nk,na pia nikuangazie pale Ziwa nyasa ambapo tuna
tarafa ya Mwambao huko upo utalii ambao kwa siku 30 sio rahisi kuumaliza utalii
wengi tunafika na kujifunza vitu vingi mazingira yake hali ya hewa vinakufanya
usitamani kutoka katika Tarafa ya Mwambao.
Upo Utalii mwingi kwenye Halmashauri yetu Misitu ya asili Ngoma bora Duniani
ya Asili inayo julikana kwa jina la Mganda na nyingine Nyingi zinazo patikana
Ludewa pekee.
Sasa unashindwaje kufika Ludewa kuja kushuhudia mengi mazuri niliyo
kuangazia? Jibu la swahi hili unapaswa kulijibu kwa vitendo kwa kuchukua hatua
za haraka kuja Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa kufanya uwekezai kuleta wageni
kutoka mataifa mbalimbali lakini watanzania wote Bara na Visiwani karibuni
Ludewa.
FURSA ZA KILIMO CHA KAHAWA LUDEWA
Wakati ukijiuliza wapi zinapatika fursa za kilimo hapa nchini Tanzania leo nakunong'oneza kwa ukaribu kuwa Halmashari ya Wilaya ya Ludew...
-
Mwenge wa Uhuru unaashiria nuru na mwanga.Uliwashwa kwa mara ya nchini Tanzania juu ya kilele cha mlima Kilimanjaro mwaka 1961. Mwenge wa ...
-
Mwenyekiti wa Halmashauri Wilaya ya Ludewa Wise Mgina Jana Machi 15, 2022 alitembelea Msitu wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa ulioko Kata y...
-
Leo Machi 21, 2022 Kaimu Mkurugenzi Wilaya ya Ludewa Bw. Gilbert Ngailo ameongoza kikao cha robo tatu ya kamati ya Wilaya ya Kupinga ukatili...